Posts

Showing posts from December, 2013

WANA WA MUNGU WAFUNGA NDOA (MOROGORO)

Image
Wana Ndoa wakiwa wamepiga Picha ya pamoja (Ndoa 26 zilizofanyika jana Tarehe 25/December/2013, EFATHA MINISTRY Morogoro) .   Wana wa MUNGU Wana Ndoa (Ndoa 26 zilizofanyika jana Tarehe 25/December/2013, EFATHA MINISTRY Morogoro) Wakionyesha Vyeti vyao vya Ndoa, Baada ya Kufunga Ndoa jana.

USIKU WA EFATHA

Image
USIKU WA EFATHA, 31 DECEMBER 2013 Kibaha Precious Centre, Tanzania katika Mji wa BWANA MUNGU WETU MKUU, Usikose Mwana wa MUNGU.

HALELUYA,MUNGU WETU NI MZURI

Image
Haleluya,... MUNGU wetu ni Mzuri, YESU wetu ni Mzuri, Tuna kila sababu ya kumwambia MUNGU Aliye BABA Yetu ASANTE, Leo Jumapili ilikuwa ni Siku nzuri sana kwa Wana wa MUNGU, Kwani BWANA wetu YESU KRISTO kupitia ROHO MTAKATIFU kwa Watumishi w ake waaminifu (kuanzia Dar es Salaam Mwenge mpaka vituo vyote) Alitupatia Chakula cha Kiroho kizuri sana, Tulilishwa vya Kutosha, YESU Anatupenda sana, ndio maana Alitupa chakula kizuri cha Kiroho ili Tutoke mahali tulipo na kwenda kwenye Utukufu, na kwenda kuwa Huru... Kwa kweli MUNGU Wetu MKUU ni Mzuri sana, Anatupenda Wanawe. Wana wa MUNGU wakitoa SADAKA ZA SHUKRANI kwa yale yote Mema Makuu ambayo MUNGU Amewatendea kwa wiki nzima, pamoja na ZAKA na Ya kutangaza INJILI pamoja na MASHANGILIO mbele ya Madhabahu ya BWANA MUNGU WETU MKUU. Kipindi cha SHUHUDA, Wana wa MUNGU walitoka mbele na Kushuhudia Mambo Makuu ambayo MUNGU WETU MKUU, MUNGU Wa EFATHA MINISTRY Aliwatendea katika Maisha yao, ATUKUZWE na KUINULIWA Aliye BWANA MUNG

UTAJUAJE UMEKOMBOLEWA?

Zab 1:3 “Kila Alitendalo litafanikiwa”, Ayub 22:28 “Nawe Utakusudia Neno nalo litathibitika kwako”. Ayub 22:21 “mjue sana MUNGU ili uwe na amani, ndivyo mema yatakavyokujia. Hatua ya kama UMEKOMBOLEWA kila unachokifanya Kinafanikiwa. UKOMBOZI ni kwa ajili ya Mafanikio yako hapa Duniani siyo Mbinguni. Usikubali kufa kabla ujafaidi maisha hapa duniani, Usikubali kujitiisha kwa adui eti kwasababu shida fulani, bali JITIISHE kwa MUNGU awezaye kukushindia shida zote. :- Apostle & Prophet Josephat Elias Mwingira.

IBADA YA JUMAPILI DEC 15, 2013.

Image
Haleluya,... MUNGU Wetu ni MZURI SANA, YESU Wetu ni MZURI SANA. Tunamshukuru BWANA wetu kwa Ibada nzuri iliyokwishamalizika, Chakula cha Kiroho kilikuwa kitamu sana, BWANA Wetu Alitulisha vema, Alitugusa katika Mahitaji yetu, Aliona Mioyo y etu Inahitaji nini, BWANA Alishuka na Kutuponya, Alishuka na Kutuweka Huru, BWANA Alikuwa nasi kupitia Mtumishi wake Mchungaji Kiongozi wa EFATHA MINISTRY Arusha, Mchungaji Tumpe Rabarn. ''Kazi ya MUNGU BABA ni KUKUTUKUZA''   ''DAI MASHANGILIO YAKO kwa kuwa Wewe ni wa UZAO WA EFATHA.'' :- Mchungaji Kiongozi Efatha Ministry Arusha, Mchungaji Tumpe Rabarn.   “Wakati adui anakaa kikao na kupanga Kukuharibu; MUNGU naye Anaongea na Watumishi wake, Anapanga KUKUINUA na KUKUTUKUZA”

KAMBI YA VIJANA KIBAHA PRECIOUS CENTRE Dec 2013

Image
Vijana wa YESU, Vijana wa Efatha siku ya Kwanza walipokuwa wakielekea Kibaha tayari kwa Kambi yenye NGUVU ya MUNGU Wetu MKUU...     Mojawapo wa Watumishi wa MUNGU Wapakwa Mafuta wa BWANA MUNGU Wetu, wanaohudumu katika Kambi hii. Mtumishi wa MUNGU akitoa Mafundisho yenye UPAKO WA NGUVU YA MUNGU Wetu MKUU kwa Vijana walioko Kambini Kibaha Precious Centre. Wana wa MUNGU Vijana wa YESU KRISTO wa Efatha, wakipokea Mafundisho na Mahubiri na Maneno yenye Hekima na Ufahamu pia wakihudumiwa Kiroho .... Efatha:Healing & Deliverance by the Blood of JESUS CHRIST... Haleluya!!!

CHAKULA CHA ROHONI

umb 29:29 “Mambo ya siri ni ya BWANA MUNGU wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu na watoto wetu milele, ili tufanye maneno yote ya sheria hii. Mambo ya siri ni ya BWANA, wana wa Israeli walipokuwa utumwani Misri walitumikishwa na kuteseka sana lakini walipokuwa njiani wakiongozwa na Musa, kwa shida ndogo walitamani kurudi Misri (walitamani mambo ya nyuma, maisha ya nyuma). Kama HUJAKOMBOLEWA unawaza mambo matatu tu, KULA, KUVAA na KULALA. Wezi wote wala rushwa, mafisadi wanaiba ili Wale, Wavae vizuri na kujenga Majumba ya kifahari ili Walale. Huyu bado hajakombolewa. :- Apostle & Prophet Josephat Elias Mwingira.

SIKU YA KUJONGEA NYUMBANI MWA BWANA (ya kumsikiliza mkalimani wetu)

Wapendwa karibuni  tujongee nyumbani mwa bwana kesho siku ya jumapili,ibada ni kama ifuatavyo: IBADA YA ASUBUHI-INAANZA SAA MOJA ASUBUHI IBADA YA MCHANA-INAANZA SAA TANO  ASUBUHI Karibuni wote!!! (wawili au watatu wakusanyikapo kwa ajili ya jina langu,nami nitakuwa pamoja nao). sasa sisi tu zaidi ya watatu je hatoshuka?????
Kwa sababu wewe sio ulioniita, Oooh Haleluya, Aliyeniita YUKO HAPO JUU na ANANIANGALIA, Jinsi ninavyotembea huku Duniani, NAKANYAGA pepo kushoto, nakanyaga jini kulia, nikitembea mapepo yanalaza mbio, wachawi wanatawanyika, Maana nina Upako wa KIFALME, na WEWE POKEAAA. :- Apostle & Prophet Josephat Elias Mwingira.
umewekwa juu pamoja naye (YESU KRISTO Bwana wetu) katika Ulimwengu wa Roho. Kwa hiyo tumeketishwa na MSHINDI, hapa hoja ni USHINDI. Kanisa la YESU KRISTO lazima liweke Records (kumbukumbu), Usiishi kama msindikizaji... lazima Uweke records, wewe ni Mshindi, Sisi tunaomwamini YESU KRISTO Tunao USHINDI. :- Apostle & Prophet Josephat Elias Mwingira.