Posts

Showing posts from February, 2014

DARASA/KONA YA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY. (Darasa linaendelea lilipoishia jana...Ubarikiwe) ''Tambua kinachokukandamiza! Wahubiri wengine watasema Kwa kuwa imeandikwa, “Hulituma Neno liwaponye, sasa nawaletea Neno la MUNGU, Amesema tena YEYE mwenyewe alichukua madhaifu na masikitiko yetu yote, …” Kwa kupigwa kwake sisi tumepona kwa hiyo pokea uponyaji! Siyo mgonjwa wala hana pepo! Miradi yake haiendelei, au watoto wanafeli shuleni, au ana matatizo katika ndoa hivyo tafuta kwa nini hayo yametokea, tafuta kiini cha tatizo! Mfano. Kuna mtu mmoja aliona maisha yake yameharibika na anakaribia kufa; alikwenda hospitali nyingi lakini hakupona, mwishoe hata hospitali wakakataa kumpokea maana hakutibika. Akaomba sana kwa MUNGU, MUNGU Akamwambia “Siwezi kukuponya mpaka uende kwa Mtumishi wangu uliyemtukana”. Alipokuja kwangu maana alikuwa ametamka maneno magumu sana juu yangu, akatubu kwa machozi; nikasikia HURUMA YA BWANA ndani yangu nikatamka Neno “Laana yako na ikuondoke”! Alikuja kwangu akiwa ameshikiliwa hawezi kutembea, baada ya laana yake kuondoka akatembea mwenyewe na UHAI ukamrudia! Ni vizuri kuelewa kinachokutesa, kumbuka “Watu wengi wanaangamia kwa kukosa maarifa” lakini kinachosababisha wakose maarifa ni kwa sababu hawajatambua UKWELI wa tatizo lake. “Utagundua SIRI na hiyo SIRI ndiyo UKWELI wenyewe na huo UKWELI Utakuweka HURU”. Omba! BWANA YESU niingize kwenye chumba cha Uchunguzi (xray); ROHO MTAKATIFU nisogeze kwenye Uchunguzi sasa nipime ee MUNGU Wangu.''

Naibariki Alhamisi Yangu!

Image

''Tabia za Upendo zikoje? 1 Wakorintho 13:1-8. Usiangalie makosa, achana na hiyo diary ya kuandika makosa, unaanda kifo cha kukua mwenyewe. MUNGU Ametupa KUSAHAU, sasa Wewe ukiandika makosa, Ukahesabu mabaya, si unajisababishia Kutosahau?, unahesabu la jana, juzi,… Watu ambao hawasalimii wenzao wanahesabu mabaya, kama uhesabu ukimwona unamwambia waooo, huo ndio UPENDO. Tengeneza MARAFIKI, usitengeneze maadui, ata kama unakumbuka, wewe ukimwona Msalimie “waoooo”.''

Naibariki Jumatano Yangu!

Image

DARASA/KONA YA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY. (Darasa linaendelea lilipoishia jana... darasa ni zuri, JIFUNZE UPATE KUJUA NINI KINAKUSHIKIRIA, NINI KINAKUTESA Ili Uweze KUKISHINDA KATIKA MAISHA YAKO) ''Zaburi 107:17 “Wapumbavu kwa sababu ya ukosaji wao na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa”. Yawezekana unapitia mateso au maumivu ambayo yametokana na maovu yaliyofanyika huko nyuma labda wazazi wako kukosea au wewe mwenyewe kutokutii mambo ambayo MUNGU Amekuagiza. Kwa sababu hiyo unateseka; asili ya makosa siyo shetani. Tuangalie kwa ukaribu watu hawa: - Daudi alipakwa Mafuta lakini alipita njia za kufuatilia mpaka alipofika mahali pa kutukuka. Yusufu naye alipakwa Mafuta na MUNGU na akatamkiwa kabisa atakuwa nani, lakini akapita mapito magumu kabla ya ndoto yake au maono yake kutimia. Jitahidi kufuatilia UKWELI ili uwekwe HURU; wapumbavu kwa sababu ya upumbavu wao hujitesa, Nafsi zao huchukia kila aina ya Chakula. Wameyakaribia malango ya kuzimu. Maanake kila unachokifanya kinakufa na wewe unaona maumivu ya kifo, lakini Biblia inasema, “Wakamlilia BWANA na dhiki zao, naye Akawaponya na tabu zao zote”'' (Itaendelea kesho, Usipitwe Mwana wa MUNGU, ndio muda wako huu wa KUWEKWA HURU).

Naibariki Jumanne Yangu!

Image

Naibariki Jumatatu Yangu!

Image

DARASA/KONA YA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY. (Darasa linaendelea pale lilipoishia wiki iliyopita... KIRI katika UFAHAMU WAKO). MUNGU Akamwambia Nabii amimine mafuta kwa Daudi; familia nzima na jamii yote ikajua huyu ndiye Mfalme. Baada ya sherehehe hawakumtambua tena; akarudi machungani; waliona kama MUNGU Amekosea kwa Daudi kupakwa mafuta. Wengi wetu tumepakwa Mafuta na BWANA kuwa Matajiri wakubwa, Wafanyibiashara wakubwa, Viongozi wakubwa lakini bado mmekaa chini, maana hakuna anayekutambua, lakini saa inakuja ya KUTAMBULIKA KWAKO, sema HALELUYA. Siku moja Daudi akatumwa na babaye awapelekee chakula ndugu zake wakiwa vitani; alipofika kule akakuta wamekumbwa na tatizo linalosumbua Taifa zima. Akajitokeza kupambana na Goliathi na akamshinda! Sasa utamshinda adui yako na Yule anayetesa familia yako na ukoo wako kwa jina la YESU. Sema HALELUYA.

Naibariki Jumatatu yangu!

Image

Haleluya,... YESU wetu ni MZURI, MUNGU wetu ni MZURI, ROHO MTAKATIFU Ni Mzuri, Ibada zimekwisha na Uwepo wa MUNGU wetu MKUU tumeuona, ROHO MTAKATIFU Akitawala, MUNGU MKUU BABA Yetu akimtumia vizuri Mtumishi wake Mama Eliakunda Josephat Elias Mwingira kutupatia Chakula kizuri cha Kiroho,... Oooh Haleluya: "Jinsi gani ya kuishi na kupata KIBALI?... Kuna Protocol/Njia/ Principal/Kanuni/Utaratibu wa Kupata KIBALI. Mfano Treni ina njia yake, bila hiyo reli treni haiwezi kwenda,... kaa kwenye reli, kaa kwenye NJIA husika ili uweze kupata hiko KIBALI, bila kukaa kwenye hiyo Reli au ukikaa nje ya Reli, huwezi kupata KIBALI..."

Image

Naibariki Ijumaa Yangu!

Image

DARASA/KONA YA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY. (Darasa linaendelea lilipoishia jana... Fungua UFAHAMU Wako) Mfano. Mwaka 1992 BWANA alinionyesha maono jinsi nitakavyokuwa. Ndani yangu niliamini lakini macho yangu yalipotizama Mazingira niliyokuwa nayo wakati huo, akili inakataa kukubaliana. Nilipofungua Biblia na kusoma inaniambia mimi Nitafanikiwa, Nitakuwa Mkuu, n.k. Kabla sijafika mwisho wangu nikasema, Niko tayari kukutumikia; mwaka 1992 Usingetamani kunisikiliza wala kuniangalia Usoni. Lakini leo MUNGU AMETIMIZA yale Aliyoahidi, leo watu wanaulizana “NI YULE YULE?” Nakutamkia kwa Neno la KINABII, “Ni wewe ambaye MUNGU anaenda kukushangaza, siku nyingi umeangalia wengine na kuwashangaa, sasa yanaenda kutokea kwako” SEMA HALELUYA!!. Hebu uwe Yusufu sasa na utunze maono hata katika Utumwa. Kuna wengi wamepoteza maono yao kwenye vitu vya kupita na sasa wamesababisha laana lakini huu ndio wakati kutambua hilo tatizo, hiyo laana na ukishagundua tatizo TUNATAFUTA DAWA; kama ni DAMU YA YESU Tutaialika; kama ni NENO LA KRISTO Tutalituma; kama ni KUKUWEKEA MIKONO Utawekewa, lazima UTOKE maana ni wakati WAKO wa Kuinuliwa, SEMA HALELUYA.

Naibariki Jumanne Yangu!

Image

DARASA/KONA YA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias MwingiraEFATHA MINISTRY. (Darasa linaendelea lilipoishia wiki iliyopita, WEKA UFAHAMU Na Uelewe...) Asili haibadiliki, labda unaweza ukasema BWANA YESU Ameshughulikia laana zote; lakini ni vema ukafahamu ni laana ipi YESU Alishughulikia na ipi amekuachia Ushughulikie nayo. Imeandikwa, “Naye alituokoa kunako laana ya Msalaba” maana alishughulikia laana ya torati! Tunapoangalia kiini cha tatizo, ndicho kitakusaidia kutoka mahali kwenda pengine, ndicho kitakachokupa CHANGAMKO la Moyo. Dunia utaiona kama ni sehemu ya shangwe! Tatizo siyo shetani bali ni ile laana iliyotupata kwa kutokutii kwetu. Shetani yeye anafuatilia tu nani amelaaniwa na kushughulika naye. Mfano. Polisi humkamata mwenye hatia na siyo kila mtu; hivyo kama huna kosa hawashughuliki na wewe ila mwenye hatia ndiye wana uwezo wa kumfuatilia na kumkamata! Kama shetani ana nguvu za kukufuatilia, maanake kuna tatizo tayari! Kama MUNGU Anasema, “Mimi nitakuwa adui wa adui zako”! Ina maana kuna mahali tunajiletea shida sisi wenyewe. “Nami nitaijua kweli nayo kweli itaniweka huru”. SEMA KWA SAUTI Iwe ni sehemu ya UKIRI wako.

Naibariki Jumatatu Yangu!

Image

YESU Ni MTAMU Jamani kuliko Chakula... Hawa Vijana Pichani nao walipata Neema ya UKOMBOZI, wao walikuwa na HOFU YA KUOA, Wanaogopa KABISA KUOA, Lakini jana Ibadani YESU ALIWAWEKA HURU... JE WEWE Hutaki kuwa HURU kwa hilo linalokutesa?, YESU YUPO ANAKUSUBIRI TU, ila Angalia Muda unakwenda Unyakuo unakaribia.

Image

Dhambi si mpaka utende, Mawazo tu yanaweza kukufanya utende dhambi...: Apostle & Apostle Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Haleluya,... YESU ni MZURI, MUNGU Wetu ni Mzuri, ... Tunamshukuru ROHO MTAKATIFU kwa kutuweka katika Uwepo wa Utukufu wa BWANA MUNGU Wetu leo katika Ibada, Ibada ilikuwa nzuri, BWANA Aliongea nasi vema, Tulikula na Kunywa Chakula kizuri cha Kiroho kutoka Madhabahuni kupitia Mtumishi wake Mkalimani wetu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira,... Oooh KIBALI ... ''Unataka kuwa Mtu wa KIBALI, basi kuwa Mtu MKWELI''

Image

Wageni kutoka sehemu mbalimbali walikuja Kumsikiliza na Kumuabudu na Kumsifu na Kumtukuza MUNGU Wa EFATHA. Je Wewe unasubiri nini?

Image