HALELUYA,MUNGU WETU NI MZURI

Haleluya,... MUNGU wetu ni Mzuri, YESU wetu ni Mzuri, Tuna kila sababu ya kumwambia MUNGU Aliye BABA Yetu ASANTE, Leo Jumapili ilikuwa ni Siku nzuri sana kwa Wana wa MUNGU, Kwani BWANA wetu YESU KRISTO kupitia ROHO MTAKATIFU kwa Watumishi wake waaminifu (kuanzia Dar es Salaam Mwenge mpaka vituo vyote) Alitupatia Chakula cha Kiroho kizuri sana, Tulilishwa vya Kutosha, YESU Anatupenda sana, ndio maana Alitupa chakula kizuri cha Kiroho ili Tutoke mahali tulipo na kwenda kwenye Utukufu, na kwenda kuwa Huru... Kwa kweli MUNGU Wetu MKUU ni Mzuri sana, Anatupenda Wanawe.


Wana wa MUNGU wakitoa SADAKA ZA SHUKRANI kwa yale yote Mema Makuu ambayo MUNGU Amewatendea kwa wiki nzima, pamoja na ZAKA na Ya kutangaza INJILI pamoja na MASHANGILIO mbele ya Madhabahu ya BWANA MUNGU WETU MKUU.


Kipindi cha SHUHUDA, Wana wa MUNGU walitoka mbele na Kushuhudia Mambo Makuu ambayo MUNGU WETU MKUU, MUNGU Wa EFATHA MINISTRY Aliwatendea katika Maisha yao, ATUKUZWE na KUINULIWA Aliye BWANA MUNGU wa miungu, YEYE Aliye MWANZO NA MWISHO, Haleluya.


Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."