Posts

Showing posts from November, 2016

Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: BWANA YESU ni RAFIKI yetu. Mfano:- Ukiwa na rafiki yako unakuwa unampenda na unatamani kumfurahisha mara zote, hivyo kama unatambua kuwa BWANA YESU ni RAFIKI yako unatakiwa UMFURAHISHE, Je utamfurahishaje? • Kwa kutenda sawasawa na maagizo yake kutoka kwa Watumishi wa Mungu, ukiwa unatamani kufanya mambo mazuri kwa ajili yake ndipo anafurahi na kama kunakitu kinakuzuilia ili usifanye vizuri anakiondoa na kukuacha ukiwa huru. • Tamani kufanya mambo mazuri kwa ajili YAKE ili YEYE akufurahie na kufungua yale yaliyofungwa katika maisha yako. Ukikosa kuzingatia kinachotoka katika MADHABAHU ya Mungu dunia itakupelekesha, unapofika hemani mwa BWANA (Kanisani) unatakiwa kutafakari yanayotoka katika MADHABAHU, usiwaze tofauti na NENO linalotoka katika MADHABAHU ya BWANA maana hautapokea chochote na mwisho wa siku utatoka kama ulivyoingia.

Image

Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: Ili tuweze kuvuta BARAKA za MUNGU kwetu ni lazima tuwe na kitu cha kumpa MUNGU, tusiende mbele zake mikono mitupu, toa nguvu zako na mali zako, baraka haziji mpaka UMEFANYA KWA BIDII ndipo wale malaika waliotumwa kwako wanapopata nguvu ya kuvuka vizuizi na kukuletea BARAKA zako. Unapokuwa na AMANI ya YESU ndipo unaweza kuzalisha vitu vingi katika maisha yako. Ili shetani akuweze kitu cha kwanza anakuondolea AMANI kwa kukukumbusha yaliyopita. Ni kweli ulikuwa mwizi, mzinzi, mlevi lakini mara baada ya kuokoka YESU alisamehe yote sasa shetani asikukumbushe ya nyuma.

Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: Mithali 8:17 " 7 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona". Bidiii ni KUWAZA, KUTAFAKARI NA KUKIRI. Anasema wampendao na kumtafuta kwa bidii watamuona, sio wale wanaosema WANAMPENDA tu ndio watakao muona ni lazima UMTAFUTE KWA BIDII. Ili mwanadamu aonekane anampenda MUNGU kuna kitu cha ziada anatakiwa akifanye, ukisha mpenda MUNGU tafuta cha kujionyesha mbele zake kwa kumtumikia kwa kutoa muda wako kwenda kuwaambia wengine habari za YESU na hapo atajua unampenda, Ili tuonekane tunampenda MUNGU lazima tushiriki yale yanayohusu UFALME WAKE hapa Duniani kama vile kupeleka injili popote Duniani kwa kujenga Makanisa na mengineyo,

Image

Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: Waefeso 1:3 " Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo; " Baraka maana yake ni nini? Baraka sio fedha tu bali mtu akikwambia umebarikiwa inamaana kuanzia mwilini mpaka Rohoni uwe umebarikiwa. Kubarikiwa ni kuwa na AMANI ya kweli ndani ya moyo wako, unapokuwa na AMANI ndipo unaruhusu mema yanakujia, unapokuwa na UCHUNGU unamfukuza YESU ndani yako. Amani ni ya muhimu sana kwako ndio maana YESU alipokuja akawakuta wanafunzi wake wamejifungia kwa hofu aliwaambia AMANI IWE KWENU, hakuwaambia mimi ndiye YESU, ukiwa na AMANI ndipo YESU anasema na wewe kwa karibu sana. Kwa nini tunatakiwa kuwa na AMANI kwanza? Kukosekana kwa AMANI ndani ya moyo wa mtu ndicho chanzo cha mabaya mengi,

Image

Waimbaji wa Efatha Ministry Mass Choir wakimsifu Mungu. Efatha Ministry Mwenge Dar es salaam.

Image

Karibuni wote katika ibada za Jumapili ya tarehe 27/11/2016 hapa Efatha Ministry Mwenge Tanzania, ibada ya kwanza inaendelea pia mnaweza kusikiliza ibada za siku ya leo kupitia www.mixlr.com/efatha-ministry . TRENET TV - YouTube Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube. YOUTUBE.COM

SHUHUDA: Naitwa Melania Shao napenda kumshukuru Mungu kwa mambo makubwa aliyonitendea. Niliokoka mwaka 2010 lakini niliingia Efatha mwaka 2011 na mwaka 2012 nilipewa nafasi ya kuwa kiongozi. Nikiwa mjamzito nilijifungua mwanangu akiwa mzima lakini baada ya miaka 3 alibadilika akawa anavimba hadi kushindwa kulana akawa hakuwi, nikampeleka hospitali na baada ya kupimwa na wataalam wakagundua haumwi chochote. Siku moja nilimleta mtu Kanisani kuombewa, Mchungaji Mdadila alipomaliza kumuombea huyo mtu akamuona mwanangu akiwa anacheza akaniuliza yule ni mtoto wa nani? nikamwambia ni wa kwangu akaniambia mbona simuoni mtoto? Nilikuwa napenda sana kumuweka urembo kichwani na kumsuka dreds Mchungaji akamnyoa nywele na kumuombea na mwanangu alipokea uponyaji na alianza kukua kama watoto wengine kwa sababu alipokuwa na miaka 5 alionekana kama mwenye miaka 3. Namshukuru sana Mungu kwa kuweza kumponya mwanangu na sasa ana miaka 10 na amerefuka. Mwaka 2013 nilibeba mimba ya mwanangu wa pili na mimba ikawa ni ya miezi 12 nikaambiwa natakiwa nifanyiwe upasuaji kwa sababu ilikuwa kila nikipimwa inaonekana kuwa mtoto amesimama na alikuwa hageuki. Mimi nilikataa kwa kuwa Baba yetu Mtume na Nabii anatufundisha kuwa watoto wetu wasitokee dirishani bali pale alipo ingilia ndipo atokee. Siku moja kukawa na ibada ya shukurani kanisani na niliombewa niliporudi nyumbani nikaenda hospitali kupima ikawa mtoto wangu amegeuka na wiki iliyofuata nikajifungua salama. Baada ya hapo mwanangu tena akawa hakui na haongei akawa mwembamba sana nikaambiwa nimpeleke India lakini nikawa nahudhuria kwenye maombi na sasa amepona na alianza kuongea akiwa na miaka 3 na sasa ana miaka 5. Namshukuru sana Mungu kwa aliyo nitendea kwani kama siyo yeye wanangu wote wangekuwa hawakui. Mtu wa Mungu usikate tamaa katika jambo unalo pitia amini ipo siku yako kwa Mungu, Mungu anaweza na atakushindia. Unachotakiwa ni wewe kutii na kufanya kile unacho elekezwa na Watumishi wa Mungu Mfano:- kuwaleta watu kwa Yesu yamkini ndiyo ikawa siku yako ya wewe kupokea uponyaji wako.

Image

English Version:TESTIMONY!! My name is Theresia Athanas, from Kilimanjaro KDC, I want to thank the Lord for the great thing that He has done in my life, this week I was called by my daughter who living in Dare s salaam when I was in Moshi, she called in and said that she had been told she had to undergo a cesarean because her child had not turned in the right direction. So I came with her to church here at Efatha Ministry Mwenge Dar and we were able to meet with Pastor Mwakisole who prayed over her and then he said we should go home and wait until she is due and that she will deliver safely. I took his word with faith knowing that it will work, at around 1 o’clock at night she starts experience pain, we rushed her to hospital where the doctors said we had to wait for till morning so that she may undergo operation at the same time she was vomiting and complaining of a lot of pain. I called Pastor Mwakisole again and he prayed for her and he said it will be well. I went outside and feel into an outburst of tears and thanked the lord , when I went back in I found that he has already given birth naturally but her child came out legs first, Pastor Mwakasole called again to know how she was and was happy to know it was all well. I really thank the Lord for delivering my daughter from the hands of death.

Image

USHUHUDA!! USHUHUDA! NAITWA THERESIA ATHANAS MOSHI Natokea Kilimanjaro KDC, wiki iliyopita nilipigiwa simu na mwanangu anayeishi Dar kuwa amepitiliza siku zake za kujifungua na kwamba ameambiwa ajiandae kwa upasuaji (Operation) kwa ajili ya kujifungua maana mtoto alikuwa hajageuka. Nikamwambia asiende kwanza hospitali anisubiri nakuja, nilipofika nikaja moja kwa moja kanisani hapa Efatha Ministry Mwenge nikaonana na Mchungaji Mwakisole, nikamweleza mwanangu ameambiwa atajifungua kwa upasuaji, Mchungaji akaomba akasema atajifungua salama kwa njia ya kawaida, ila msimpeleke hospitali hadi uchungu utakapoanza. Uchungu ulipoanza tukampeleka hospitali, manesi waligomba kwa nini tumemchelewesha, maana alitakiwa kuwahi kwa ajili ya upasuaji, mimi nikamwambia mwanangu hatajifungua kwa upasuaji. Wakasema haiwezekani maana mtoto hajageuka na mtoto akiwa katika hali hii huwa tunafanya operation ili kuokoa maisha ya mama na mtoto hivyo ni lazima apasuliwe. Nikampigia Mch. Mwakisole nikamweleza, akasema niweke simu kwenye tumbo aongee na mtoto, nikaweka akaomba. Baada ya hapo hali ya mwanangu ikawa mbaya akaanza kutapika hadi, kuishiwa nguvu. Akakimbizwa chumba cha upasuaji, mimi nikatoka nje nikimshukuru Mungu. Katika hali isiyo ya kawaida mtoto akaanza kutoka haraka kwa miguu akamalizia na kichwa, hadi manesi wakashangaa na wao walikiri kuwa ni Mungu aliyefanya. Wakaniambia usiache kumshukuru Mungu kwa jambo hili. Ndio maana nipo mahali hapa kumshukuru Mungu maana alisema kupitia Mtumishi wake Mtume na Nabii Josephat E. Mwingira kuwa sio sawa kujifungua kwa operation, bali mtoto anatakiwa kutoka kupitia njia aliyoingilia. Namshukuru pia Mchungaji mwakisole kwa kuwa pamoja nami, Mungu ambariki sana. MUNGU HASHINDWI

Image

PICHANI: Waimbaji wa Efatha Ministry Chipkizi wakimtumikia Mungu katika Ibada ya pili inayoendelea hapa Efatha Ministry Mwenge Dar

Image

MCHUNGAJI DAVID MWAKISOLE: SOMO: SIRI YA BARAKA ZA MUNGU WAPI ZILIPO: Kumbukumbu la torati 28:1 "takuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani" . Baraka sio kuwa na fedha peke yake kwani unaweza kuwa na fedha na bado ukawa umelaaniwa, baraka ni kuwa karibu na MUNGU ili uweze kupokea vya kwake. Asili ya baraka zote ni YESU na ili tuweze kuzipata hizo baraka ni lazima tuachane na mambo yote yanayo haribu uhusiano wetu na YESU na kutuweka mbali na MUNGU. Inawezekana ni dhambi ya uvivu, uvivu katika mambo ya MUNGU ni kikwazo kikubwa cha kupokea baraka zetu toka kwa MUNGU.

MCHUNGAJI DAVID MWAKISOLE: SOMO: SIRI YA BARAKA ZETU WAPI ZILIPO: Baraka maana yake ni kinyume cha laana, ukiambiwa umebarikiwa maana yake hujalaaniwa na ukiambiwa umelaaniwa maana yake kwako hakuna baraka. Laana imekuja baada ya mtu kumkosea MUNGU, mtu akikwambia umelaaniwa maana yake uko mbali na MUNGU na akikwambia umebarikiwa maana yake uko karibu na MUNGU. Asili ya baraka zote ni MUNGU mwenyewe, hutaweza kuziona baraka mpaka umepatana na MUNGU na ukifarakana naye tu utaanza kuona laana zikikufuata na kila unachokifanya kinaharibika.

Image

Karibuni wote katika ibada za Jumapili hapa Efatha Ministry Mwenge Dar es salaam Tanzania, ibada ya kwanza inaendelea pia mnaweza kusikiliza ibada za siku ya leo Live kupitia Online Radio www.mixlr.com/efatha-ministry .

Tne Leaders Service is in session at Efatha Ministry Eldoret. In whichever position you have been given to serve; serve it well, for the Glory of GOD. Pastor Godson Mmari. EFATHA MINISTRY's photo.

Image

Waimbaji wa Efatha Ministry mass choir wakisifu Mungu katika ibada ya kwanza leo Jumapili Efatha Ministry Mwenge,

Image

Karibuni wote katika ibada ya kwanza hapa Efatha Ministry Mwenge Dar es salaam Tanzania. Popote ulipo unaweza kusikiliza ibada za siku ya leo LIVE kupitia www.mixlr.com/efatha-ministry