Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: Mithali 8:17 " 7 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona". Bidiii ni KUWAZA, KUTAFAKARI NA KUKIRI. Anasema wampendao na kumtafuta kwa bidii watamuona, sio wale wanaosema WANAMPENDA tu ndio watakao muona ni lazima UMTAFUTE KWA BIDII. Ili mwanadamu aonekane anampenda MUNGU kuna kitu cha ziada anatakiwa akifanye, ukisha mpenda MUNGU tafuta cha kujionyesha mbele zake kwa kumtumikia kwa kutoa muda wako kwenda kuwaambia wengine habari za YESU na hapo atajua unampenda, Ili tuonekane tunampenda MUNGU lazima tushiriki yale yanayohusu UFALME WAKE hapa Duniani kama vile kupeleka injili popote Duniani kwa kujenga Makanisa na mengineyo,

Comments