Mchungaji David Mwakisole: SOMO: ASILI YA BARAKA ZETU NI KATIKA KRISTO YESU: BWANA YESU ni RAFIKI yetu. Mfano:- Ukiwa na rafiki yako unakuwa unampenda na unatamani kumfurahisha mara zote, hivyo kama unatambua kuwa BWANA YESU ni RAFIKI yako unatakiwa UMFURAHISHE, Je utamfurahishaje? • Kwa kutenda sawasawa na maagizo yake kutoka kwa Watumishi wa Mungu, ukiwa unatamani kufanya mambo mazuri kwa ajili yake ndipo anafurahi na kama kunakitu kinakuzuilia ili usifanye vizuri anakiondoa na kukuacha ukiwa huru. • Tamani kufanya mambo mazuri kwa ajili YAKE ili YEYE akufurahie na kufungua yale yaliyofungwa katika maisha yako. Ukikosa kuzingatia kinachotoka katika MADHABAHU ya Mungu dunia itakupelekesha, unapofika hemani mwa BWANA (Kanisani) unatakiwa kutafakari yanayotoka katika MADHABAHU, usiwaze tofauti na NENO linalotoka katika MADHABAHU ya BWANA maana hautapokea chochote na mwisho wa siku utatoka kama ulivyoingia.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."