DARASA/KONA YA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias MwingiraEFATHA MINISTRY. (Darasa linaendelea lilipoishia wiki iliyopita, WEKA UFAHAMU Na Uelewe...) Asili haibadiliki, labda unaweza ukasema BWANA YESU Ameshughulikia laana zote; lakini ni vema ukafahamu ni laana ipi YESU Alishughulikia na ipi amekuachia Ushughulikie nayo. Imeandikwa, “Naye alituokoa kunako laana ya Msalaba” maana alishughulikia laana ya torati! Tunapoangalia kiini cha tatizo, ndicho kitakusaidia kutoka mahali kwenda pengine, ndicho kitakachokupa CHANGAMKO la Moyo. Dunia utaiona kama ni sehemu ya shangwe! Tatizo siyo shetani bali ni ile laana iliyotupata kwa kutokutii kwetu. Shetani yeye anafuatilia tu nani amelaaniwa na kushughulika naye. Mfano. Polisi humkamata mwenye hatia na siyo kila mtu; hivyo kama huna kosa hawashughuliki na wewe ila mwenye hatia ndiye wana uwezo wa kumfuatilia na kumkamata! Kama shetani ana nguvu za kukufuatilia, maanake kuna tatizo tayari! Kama MUNGU Anasema, “Mimi nitakuwa adui wa adui zako”! Ina maana kuna mahali tunajiletea shida sisi wenyewe. “Nami nitaijua kweli nayo kweli itaniweka huru”. SEMA KWA SAUTI Iwe ni sehemu ya UKIRI wako.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."