Posts

Showing posts from February, 2015

SHUHUDA Jumapili tarehe 22/2/2015

Image
Nilikuwa na Kibao cha Marufuku kwamba Siwezi kufaulu, lakini baada ya Kuomba na Kuvunja Kibao hicho, Nimefaulu na Nimepata DIVISION ONE. Ester David Msimbi: Napenda kumshukuru MUNGU, katika kusoma kwangu nimekuwa nikifanya vizuri lakini nilikuwa sishiki Nafasi ya Kwanza, nilikuwa namaliza Kisutu Sekondari, wakati huo nilikuwa na mambo yangu mengi ya uongozi, nilikuwa sifanyi vizuri, nilipokuwa nafanya Mitihani nilikuwa sipati zile Division zinazo takiwa. Lakini baada ya Mafundisho ya Mchungaji wangu Mama Mdadila aliposema kuna “KIBAO cha Marufuku” kimeandikwa mbele yangu kwamba Sitafaulu, akasema “TUKIVUNJE” kile kibao, na baada ya Kuomba na Kuvunja kile kibao MUNGU Aliniona na Kunisaidia, nimepata Division ONE. Na kuna maneno magumu kutoka kwa baba yangu mzazi alinitamkia, ya kwamba nitafeli nitapata ziro - ziro lakini MUNGU alijiinua kwangu na kunipa Kibali kwa Mwaka huu wa (Mtembeo Wa MUNGU Kwa Wale Alio Waridhia) nimepata Divison One. Lakini hii yote ni kwa sab

IBADANI JUMAPILI TAREHE 15/2/2015

Image
USHUHUDA Glory Samweli natokea Eneo la Sayuni napenda kumshukuru Mungu kwa ajili ya Baba Josephat pamoja na Maaskofu wangu wote, napenda kumshukuru Mungu amenipa Ndoa katika familia yetu tulikuwa hatuolewi ila kwa sasa ni mimi ambaye ni wa kwanza kuolewa na kuwa ndoa katika familia yetu. Nilijifunza, Baba Mtume na Nabii alisema JIFUNZE kupata maisha ya Ushuhuda, sasa nimeolewa na Ndoa yangu imefanyika mwaka jana tarehe 23/8/2014. Ilikuwa sikumoja Baba alituambia tucheze ngoma za asili nilikuwa nina maisha magumu lakini nilikuwa nacheza huku nikimwambia Mungu nataka nikuone, na kweli Mungu aliniridhia Baba alinipa shilingi 10,000 nikaanzishe biashara, ila nilivyofika nyumbani nikamwambia Roho Mtakatifu hii hela haitoshi nataka unipe nyingi zaidi ya hii. nikaja kutoa fungu la kumi na sadaka. Siku ya pili ilipofika akaja mtu akasema nataka tufanye biashara, akanipa hela akaniambia chukua hii hela utanirudishia kidogo kidogo. Namshukuru Mungu sasa nina cafe yangu

IBADA KUU JUMAPILI TAREHE 8/2/2015

Image
SHUHUDA ANAMSHUKURU MUNGU KWA KUFAULU MASOMO Naitwa Cosmas Peter, wa eneo la Shalom, Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kumaliza chuo kikuu na kufaulu mitihani ya CPA, leo niko mbele yenu namshukuru Mungu, mwaka 2009, nilimaliza chuo kikuu huria, nilifanya mitihani yangu ya CPA lakini sikufanya vizuri masaomo yote. Baada ya hapo nilianza masomo ya kukulia wokovu, ubatizo wa maji mengi na Roho Mtakatifu. siku moja Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira alisema , ukitaka k utoka mahali ulipo dhamiria moyoni mwako, baada ya hapo niliondoka na kutoa pesa zilizokuwa kwenye akanti yangu ya benki na kutoa madhabahuni. Baada ya kutoa hizo pesa zote miezi mitatu baadaye nilipata pesa nyingine kwaajili ya ada ya chuo, ndipo 2014 nilianza tena chuo na kufanya mitihani yangu ya CPA na kufanya vizuri masomo yote, kwahiyo ndani ya mwaka mmoja nikafanikiwa kumaliza masomo ya CPA. Hivyo namshukuru Mungu kwa yote aliyonitendea. Kwa hiyo nawasihi wana wa Mungu washike neno linaloto

JAMII

Image

IBADA KUU JUMAPILI TAREHE 1/2/2015 EFATHA MWENGE

Image
Kiongozi ibada ya sifa mass choir, Anna akiongoza mass choir kumwabudu Mungu wetu Ibadani. Mch. Betson Kikoti, Mchungaji kiongozi Efatha Ministry Kenya, alihudumu Ibada ya kwanza, hakika Mungu wetu ni Mwema. Mch Mese Komba wa Efatha Mbauda Arusha, akihudumu katika Ibada ya Pili Efatha Mwenge Dar es salaam   Mimi ni Mtume Ruffas Christeen kutoka Pakistani Nilikuwa katika kufunga na kuomba kwa siku 40 kwa ajili ya kutaka kumtafuta Baba wa kiroho ndipo Mungu akanionesha Mtume wake, Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, ambaye niliona habari zake kupitia mtandao wa Internet, Mungu akanimbia nije Tanzania ndipo nitakapomuona yeye (Mungu) kupitia Mtumishi wake Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, sasa ninafuraha kuwa nimempata Baba ambaye ni Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, na mimi sasa ni sehemu ya Huduma ya Efatha kule Pakistan  Mtume Ruffas Christee kutoka Pakistan akisalimia kanisa hapa Efatha Mwenge, ni mtumishi aliyeona nee