IBADANI JUMAPILI TAREHE 15/2/2015

USHUHUDA
Glory Samweli natokea Eneo la Sayuni napenda kumshukuru Mungu kwa ajili ya Baba Josephat pamoja na Maaskofu wangu wote, napenda kumshukuru Mungu amenipa Ndoa katika familia yetu tulikuwa hatuolewi ila kwa sasa ni mimi ambaye ni wa kwanza kuolewa na kuwa ndoa katika familia yetu. Nilijifunza, Baba Mtume na Nabii alisema JIFUNZE kupata maisha ya Ushuhuda, sasa nimeolewa na Ndoa yangu imefanyika mwaka jana tarehe 23/8/2014.
Ilikuwa sikumoja Baba alituambia tucheze ngoma za asili nilikuwa nina maisha magumu lakini nilikuwa nacheza huku nikimwambia Mungu nataka nikuone, na kweli Mungu aliniridhia Baba alinipa shilingi 10,000 nikaanzishe biashara, ila nilivyofika nyumbani nikamwambia Roho Mtakatifu hii hela haitoshi nataka unipe nyingi zaidi ya hii. nikaja kutoa fungu la kumi na sadaka. Siku ya pili ilipofika akaja mtu akasema nataka tufanye biashara, akanipa hela akaniambia chukua hii hela utanirudishia kidogo kidogo. Namshukuru Mungu sasa nina cafe yangu (mgahawa) na unajulikana sana ipo maeneo ya Masaki, namshukuru Mungu sasa nina jina kubwa.
 Naitwa Lucy Mtege wa Ubungo Maziwa, namshukuru Mungu kwa binti yangu kujifungu salama , jumaplili nilikuja na binti yangu alikuwa anasumbuliwa na pepo la ngono baada ya maombi binti yangu alitoka kwenye kiti akakaa chini akawa anajisikia vibaya na wahudumu walikuja kumchukua wakambeba na walimtoa nje na kumwingiza katika chumba kimoja na ndani ya kile chumba kulikuwepo na madaktari walimwombea na kupona mguu wake aliokuwa analalamika mama mguu unauma, lakini baada ya muda kuombewa maombi akawa mzima, na hakusikia tena yale maumivu ya mguu, na baada yakuachilia mguu mwanangu akaanza kusikia uchungu na kusaidiwa na madaktari akajifungua salama hapahapa kanisani mtoto wa kike anaitwa Eliakunda .

 TANGULIZA MAMBO MUHIMU KWANZA?
Jambo moja muhimu wewe unatakiwa uwe wa muhimu ufanye mambo ya muhimu, hakuna mtu anayefanya mambo ya ovyo ovyo alafu akawa mtu muhimu, fanya mambo ya muhimu ili uwe mtu muhimu. Unaweza ukaona mke wako, gari, kazi, nyumba na watoto ni wa muhimu kumbe sivyo kuna jambo ambalo unatakiwa kulifanya muhimu ndipo vitu vyote vitaonekana muhimu mfanye Mungu wa muhimu kwanza ndivyo vitu vyote kwako vitaonekana vya muhimu. Utafuteni kwanza ufalme wake na vingine vyote mtazidishiwa.
 Efatha mass choir wakimsifu na kumwabudu Mungu Ibadani, nifuraha na amani kumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli. Karibu uungane nasi kila Jumapili

Comments