IBADA KUU JUMAPILI TAREHE 8/2/2015

SHUHUDA
ANAMSHUKURU MUNGU KWA KUFAULU MASOMO
Naitwa Cosmas Peter, wa eneo la Shalom,
Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kumaliza chuo kikuu na kufaulu mitihani ya CPA, leo niko mbele yenu namshukuru Mungu, mwaka 2009, nilimaliza chuo kikuu huria, nilifanya mitihani yangu ya CPA lakini sikufanya vizuri masaomo yote. Baada ya hapo nilianza masomo ya kukulia wokovu, ubatizo wa maji mengi na Roho Mtakatifu. siku moja Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira alisema , ukitaka kutoka mahali ulipo dhamiria moyoni mwako, baada ya hapo niliondoka na kutoa pesa zilizokuwa kwenye akanti yangu ya benki na kutoa madhabahuni. Baada ya kutoa hizo pesa zote miezi mitatu baadaye nilipata pesa nyingine kwaajili ya ada ya chuo, ndipo 2014 nilianza tena chuo na kufanya mitihani yangu ya CPA na kufanya vizuri masomo yote, kwahiyo ndani ya mwaka mmoja nikafanikiwa kumaliza masomo ya CPA. Hivyo namshukuru Mungu kwa yote aliyonitendea. Kwa hiyo nawasihi wana wa Mungu washike neno linalotoka madhabahuni na kulitendea kazi ndipo watakapoona matokeo yake.
  JOHN MASENGA (APATA UPONYAJI DHIDI YA UGONJWA WA TEZI DUME)
Leo ninatoa ushuhuda wangu nilikuwa nasumbuliwa na tezidume ambalo lilikuwa linanisumbua kwa mda mrefu madaktari walisema nifanyiwe upasuji lakini mimi na mke wangu tukasema daktari ni MUNGU hivyo tukaingia kwenye maombi, nilivyoenda kupima Daktari aliniambia sina tena tatizo hilo, yaani ni alinikuta ni Mzima kabisa hivyo namshukuru MUNGU.
 Efatha mass choir wakimsifu na kumwabudu Mungu wetu Ibadani leo.
Mch. David Mwakisole Mchungaji kiongozi Mwenge akifundisha Neno Ibada ya pili Somo lenye Kichwa :
MLANGO UMEFUNGULIWA MBELE YAKO NA WAPO MAADUI WANAOKUZUIA KUINGIA. 1Kor 16:5-9

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."