SOMO: IMANI;
Waebrania 11:1 “Basi imani ni kuwa na HAKIKA ya mambo YATARAJIWAYO, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” Imani ni nini? Imani ni hakika ya mambo yatarajiwayo, kile unachokitarajia ndiyo tunaita Imani.
Imani huja kwa kusikia lakini inategemea unasikia nini wewe? Siyo kila unachokisikia kinataleta imani, bali kwa kusikia Neno la Mungu ndipo Imani inajengwa.
Tunasikia Neno la Mungu kupitia kwa watu wanaomjua Mungu, hivyo unaposikia Neno la Mungu kwa umakini na ukatenda sawa sawa na kile Neno linasema unapata uhakika wa kile ulichokisikia, hii ndiyo Imani. Watu wengi leo hii wanakwenda Kanisani wanasema wanamwamini Mungu lakini hawaamini kile wanachokisikia kutoka kwa Watumishi wa Mungu, watu hawa ni ngumu sana kupata Imani.
Kama unataka kuwa na imani sikiliza Neno la Mungu kutoka kwa Watumishi wake na utende sawa sawa na Neno linavyosema.
© Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira - Efatha Ministry.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."