Wana wa Israel ili waifikie nchi ya Ahadi ambayo Mungu aliwaahidi haikuwa rahisi, walikaa jangwani kwa muda wa miaka 40 walipitia vikwazo vya kila aina japo kuwa ulikuwa ni Unabii. Walipo ingia nchi ya Ahadi walikutana na mapambano na vita lakini ulikuwa ni Unabii.
Watu wengi siku hizi hawapendi kujifunza au kusikia Neno la Mungu litakalo wasaidia wao kutenda sawa na Mapenzi Ya Mungu bali wanapenda kusikia Unabii tu, hivyo kuwasababisha kuhangaika huku na kule ili kutafuta Unabii. Unapaswa kujua kuwa Unabii upo ili kukutia moyo na kukuwezesha wewe kusonga mbele lakini si kukupa STAHIKI yako, Imani yako ndiyo itakufanya upokee STAHIKI yako kutoka kwa Mungu, kwa sababu Imani yako itakupa Tumaini la kungoja kile unacho kiamini mpaka kitakapo tokea.
Tamani kujifunza Neno la Mungu litakalo kupa Imani na Tumaini la kungoja kile Mungu amekuahidi na si kusikia Unabii ambao hata ukichelewa kutimia kwako utakusababisha wewe kuhangaika huku na kule.
© Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira - EFATHA MINISTRY.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."