Ni vizuri ukaelewa namna ya kuwa MWANA halisi wa Mungu, unatakiwa kuishi maisha MATAKATIFU ili wakati wa hukumu usihukumiwe. Ni kweli ulizaliwa katika familia ya wanafiki, wezi, na waongo lakini unapookoka unatakiwa UJIFUNZE NENO la Mungu ili kuondokana na hali hiyo, pasipo kujifunza hizo tabia hazitaondoka kwako.
Jifunze kuwa kiumbe kipya, jifunze KUTAMKA maneno mazuri na kutenda mambo MEMA uwe kama Mungu, ili Ibilisi asikuweke hatiani. Unaweza kufanya uovu katika hali ya kujificha lakini tambua Ibilisi anakuona na Mungu anakuona. Hakikisha unatenda HAKI na kuwa mtu MWEMA mahali popote ulipo na kwa kufanya hivyo utakuwa MSHINDI katika kila ulifanyalo.
 ©Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments