Mungu yupo tayari kukusaidia kwa yote unayohitaji ili kufanikisha Mipango na Ndoto zako. Ataondoa kila kikwazo, kipingamizi, uadui na hali ya kushindwa inayokukalibia ili uweze kutimiza mambo ambayo umeyapanga yatokee katika Mwaka huu wa USHINDI, kwa sababu kufanikiwa kwako ndiyo Furaha ya Mungu.
Kila unapofanikiwa katika Maisha yako unasababisha Ufalme wa Mungu Kuongekezeka, Kustawi na Kuleta UTUKUFU na SIFA kwa Mungu, ndiyo maana anasema “Eleza mambo yako upewe haki yako”, Mafanikio ya Wana wa Mungu ni sehemu ya Haki, Urithi na Imani yao kwa Mungu. Kwahiyo katika Mwaka huu wa USHINDI usikate tamaa, fanyia Kazi Maono yako Ili Mungu aweze kukuwezesha zaidi na zaidi.
©Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.


Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."