IBADA YA MKESHA WA MWAKA 2019.
#MWAKA huu hakutakuwa na mateso juu yako maana BWANA atakomesha mateso yako, Nahumu 1:9 “Mnawaza nini juu ya BWANA? Yeye atakomesha kabisa; mateso hayatainuka mara ya pili.” Kama kuteseka umeteseka vya kutosha mateso hayatainuka tena kwako.
   - #MWAKA huu patakuwa na MTIKISIKO wa kushangaza katika Maisha ya wanadamu ili kuruhusu UTUKUFU wa Mungu kuwafunika wale Wampendao, Mtikisiko huu utakuwa ni wa kuondoa yale yanayozuia wana wa Mungu wasipokee Baraka za Mungu.
• MTIKISIKO huu utasababisha MEMA ya Milele yakujilie wewe Mwana wa Mungu.
• Hagai 2:6 “Kwa maana BWANA wa majeshi asema hivi, Mara moja tena, ni kitambo kidogo tu, nami nitazitikisa hizo mbingu, na hii nchi, na bahari, na nchi kavu;” Huu ni WAKATI wako ambao Mungu anaenda kukutikisia yale yanayokuzuia kwenda mbele, atatikisa ili MATAKATIFU yake yakujilie.
• BWANA atakufanya #RUNGU lake, Yeremia 51:20 “Wewe u rungu langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunja-vunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;” Neno lako litakuwa na NGUVU, utakapo litamka LITATENDA kwa adui zako, utakapo tamka neno utasababisha adui zako Wapigwe.
• Kipindi hiki HAKUNA mchawi atakatiza mbele yako, kipindi hiki ndicho ambacho utatamka neno juu ya ukoo wako na mizimu na matambiko yanayo kufuatilia yatakimbia. Matambiko na mizimu inasababisha wewe usisonge mbele.
   - BWANA atabadilisha Moyo wako uliyo na hali ya kushindwa na roho yako iliyo na hali ya kukata tamaa nawe utapewa roho na moyo mpya ili upate KUSHINDA kwa Jina la Bwana kila uendapo. Ezekiel 36:26 "Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama."
   :- Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments