IBADA YA KWANZA TAREHE 23/12/2018 EFATHA MINISTRY MWENGE.
MTUMISHI WA MUNGU MAMA ELIAKUNDA MWINGIRA.
JINSI YA KUTUNZA NGUVU YA MUNGU KWA WATAKATIFU;
      • Yakobo 1:22-23 “Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo.” Ili uweze kutunza Nguvu ya Mungu kwako ni lazima uwe Msomaji wa NENO la Mungu na utende sawa sawa na NENO linavyosema.
      • Ondoa HASIRA kifuani mwako ili uweze kutenda haki ya Mungu, Yakobo 1:20 “kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.” ukiwa na hasira hautaweza kufanya haki ya Mungu.
      • Ondoa MASHAKA ndani yako maana mwenye mashaka hajakamilika, Yakobo 1:6-8 “Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku......”
Unapokuwa na Mashaka katika jambo lolote ulilosema na Mungu hautalipokea, mwisho wa siku utaishia kusema kuwa hakuna MUNGU, mashaka ni adui wa kupokea BARAKA za Mungu na yale Aliyokuahidi.


Comments