SOMO: SAFARI YA IMANI.
Mwamini hahukumiwi na Ibilisi bali na Mungu, kama umeokoka na unatandikwa na Ibilisi tatizo siyo Ibilisi maana hana mamlaka ya kukuhukumu, ukitaka kujua hili vizuri soma kitabu cha Ayubu. Baya likikutokea fikiri usiombe mpaka utakapo jua tatizo ni nini. Ukiona Watakatifu wanapitia magumu usiwahukumu maana hujui kwa nini wanapitia hayo.
Usimuhukumu mtu ambaye haujui Mungu ana mpango gani na yeye huenda huyo mtu ndiye atakayekuombea kesho.
1Petro 2:3 “Ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.” Lazima umuonje Mungu, katika safari ya Imani hapo ndipo unaweza kuonja uzuri wa Mungu lakini nje ya safari ya Imani kamwe hautaweza kuuonja UZURI wa Mungu.
: - Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."