Yeremia 23:23 “Mimi ni Mungu aliye karibu, asema BWANA, mimi si Mungu aliye mbali.” Je! Umewahi kujiuliza kuwa, mara nyingi umekuwa ukiomba na hauoni majibu wakati Mungu amesema kuwa YEYE ni Mungu aliye karibu na wewe?
Kwa nini hajibu maombi yako? Unapaswa kuchunguza mahusiano yako na YEYE yakoje, YEYE ni Mtakatifu; Je! Unaishi katika Utakatifu? YEYE Anasamehe, Je! wewe Unasamehe wale wanaokukosea? 
Mungu anataka upokee Mema kutoka kwake, hivyo JICHUNGUZE wewe mwenyewe kuwa je! Unatii sheria zake? 

Chunguza Moyo wako leo na uamue kugeuza njia zako ili upate kumuona Bwana katika maisha yako, ACHA KUJIFARIJI.
   :- Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments