SOMO: TAMKA NENO.

Unapotamka NENO, unasababisha Ulimwengu wa roho KUITIKA usemacho na kuruhusu Dunia kutekeleza. Tamka neno ili kuruhusu ulimwengu wa roho kulichukua na kuelekeza duniani litekelezwe. Ukielewa siri hiyo utaifurahia dunia, kwani vilivyoko vina kazi ya KUTEKELEZA kile roho amesema; kiwe chema au kibaya. 

Pumzi yako ina nguvu ya roho, hivyo chochote utakachosema ni lazima ulimwengu wa roho uitike ili kutekeleza. Ukisema hasi au neno baya kuhusu Maisha au Mazingira yako, shetani huchukua hilo neno na kulifanyia kazi ili kukuletea ubaya.

Ukiona ubaya unakujilia au mazingira mabaya yanayokunyima furaha au kukuondolea Amani, usitamke ile hali mbaya, bali kiri kama NENO linavyosema ili kusababisha hali CHANYA kujitokeza kwenye Maisha yako. Jitahidi kukiri NENO la Mungu wakati wote ili kuruhusu ROHO wa Mungu kulithibitisha upate kupokea Ahadi za Mungu.

: Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira - Efatha Ministry.

Comments