SOMO: NGUVU YA MUNGU.
Matendo ya Mitume 1:8 "Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi". Anataka tuwe MASHAHIDI katika Dunia hii, kuanzia hapa tulipo, kule tunakokwenda, tunakofanya Kazi, kwa Majirani zetu na mahali ambapo hatuwezi kufika lakini tunaweza kuwa Mashahidi huko. Tunakuwa Mashahidi wa YESU KRISTO kwa sababu Ushahidi huo ni HABARI NJEMA, nje ya Ushahidi wa YESU KRISTO ni Habari Mbaya.
YESU peke yake ndiye Anayeweza kukupeleka MBINGUNI, KUPONYA magonjwa, KUKUKOMBOA katika umaskini, KUKUSAIDIA Kuishi na Mke kwa Amani maana pasipo YEYE ni vurugu, Ndoa nyingi ni vurugu na kilio kila siku, watoto wanateseka ni kwa sababu hakuna HABARI NJEMA huko ndani. Popote YESU alipo kuna AMANI kwa sababu YEYE ni Mfalme wa Amani, ni MSHAURI Mkuu anaweza kukushauri wapi pa kwenda na nini cha kufanya, anajua jana yako na kesho yako. YESU anajua nini kilitokea ulipozaliwa na kwa nini ulipitia hayo uliyopitia. Mambo mengine yanatokea huelewi kwa nini yanatokea ila YESU Anajua kwa nini yanatokea na ATAKUSAIDIA, YEYE alikuwepo kabla ya uumbaji, kabla hujazaliwa na Ataendelea KUWEPO.
   : Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.



Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."