Mungu alimpenda mwanadamu tangu hapo Mwanzo, na Ahadi yake ya kwanza kwa huyo mwanadamu ni Baraka. Mwanzo 1:28 “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.”
Unapokuwa maskini ina maana kuwa haueleweki ni Mungu yupi unayemtumikia; kwani ni dalili ya kwamba upo karibu na shetani kuliko Mungu anaye Bariki. Neno linasema, “Ukabarikiwe na siyo ukawe fukara” na tena ukatawale kila kiumbe chenye uhai, ina maana kuwa ukatawale kila kitu.
Kwa Mungu hakuna maskini, kinachotesa Watakatifu wengi ni kutokutambua wao ni wa kinanani katika UFALME wa Mungu. Kuna watu wameokoka miaka mingi lakini Maisha yao ni duni mpaka shetani anawashangaa, wakati kwa Mungu kuna utele.
Wewe uliyeokoka jitambue wewe ni nani kwa BABA yako wa Mbinguni ili upate KUMILIKI vile alivyokukusudia hapa Duniani.
   : Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."