IBADA YA JUMAPILI Tarehe 11/March/2018.
MTUMISHI WA MUNGU MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA:

MWAKA huu Mungu alisema nasi kuwa ni Mwaka wa NGUVU kwa sababu Mungu ATATUWEZESHA kuipata hiyo NGUVU, yaani kwa maana nyingine huu ni Mwaka wa UWEZESHO, Mungu anataka tuwe na NGUVU katika Maeneo yote.

Matendo 1:8 “Lakini mtapokea NGUVU, akiisha kuwajilia JUU YENU ROHO MTAKATIFU; nanyi mtakuwa Mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.” Unapaswa KUMJUA yule Anayebeba hiyo NGUVU kwa sababu ukimpuuza kamwe HUTAWEZA kupokea kile unachotakiwa Kukipokea, MBEBA Nguvu ni wa muhimu sana. 

Yule ANAYETUMA ni wa muhimu zaidi lakini YEYE Amekwisha kutuma ili UIPOKEE, hivyo wewe unapaswa kumjua YEYE ANAYEBEBA na ndiyo maana akasema kuwa “Lakini mtapokea NGUVU, akiisha kuwajilia JUU YENU ROHO MTAKATIFU;” hii ina maana kuwa hutaweza kupokea Nguvu kama Asipokujilia huyo ROHO MTAKATIFU lakini Akija utakuwa UMEPOKEA kile unachokihitaji.

Comments