WEWE ambaye Umeokoka shika WOKOVU wako sawasawa kwani wako watu ambao Wanakuhitaji, wewe ni NURU na wengine wanatakiwa KUIONA Nuru yako. Je Unaang’aza au watu wakikuangalia wanaona giza?.
Mimi ni BALOZI wa Yesu hivyo popote ninapopita Yesu ANAONEKANA Ndani yangu na watu huniuliza wewe ni Mtumishi wa MUNGU? Je wewe UNAMTANGAZA Yesu katika Maisha yako na popote unapopita watu wanaseme wewe ni Mtumishi wa MUNGU au watu wanasema kama Wokovu wenyewe ndio huu basi, kwa sababu ya TABIA zako? Hakikisha TABIA yako INAMTANGAZA Yesu na Mwenendo wako UNAMHUBIRI Kristo sawasawa, uwe Barua inayosomeka vizuri, Wewe ni BALOZI wa Yesu watu wakikuona wanatakiwa wamuone YESU.

   :- Mtumishi wa MUNGU Mama Eliakunda Josephat Mwingira (EFATHA MINISTRY).

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."