SOMO: NGUVU YA MUNGU.

Chochote hapa Duniani kinafanya KAZI kwa kutumia NGUVU, ili ufanye Kazi unahitaji NGUVU na huwezi Kuolewa kama huna Nguvu ya KUVUTIA Waoaji KUKUOA, vile vile huwezi kupata Mtoto kama huna Nguvu ya KUKUWEZESHA Kupata Mtoto.

Ipo NGUVU inayosababisha vitu VITOKEE ndio maana unaona wanasiasa wanatumia nguvu kupata nguvu, wengine wanatumia wachawi kupata nguvu kwa sababu wachawi wana nguvu ya uovu, wakiona haiwasaidii wanatumia Polisi kupata nguvu.

Unapotumia nguvu ya UOVU hutaenda MBINGUNI. Yeyote anayetoa rushwa au kuiba mali au nafasi ya mtu mwingine anaharibu Maisha ya huyo mtu na ni muuwaji na wauwaji hawataingia Mbinguni. Chochote utakachowafanyia watu wengine Mungu atakufanyia vivyo hivyo. 

Acha WAOVU waendelee kufanya UOVU wao na WATAKATIFU waendelee kuwa WATAKATIFU na Mungu aliye hakimu wa Haki atahukumu kwa haki.

Usifanye UOVU kwa sababu Mungu atakuhukumu na atakutupa kuzimu. Jehanamu ni sehemu ya HATARI sio VEMA wewe ukaingia huko, ni sehemu MBAYA sana na ina HARUFU MBAYA sana, ni kwa ajili ya waovu.
   :- Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.


Comments