SOMO: KUTAMBUA ADUI ANAYEKUTAFUNA.
Adui mkubwa wa mtu ni yeye mwenyewe. Mithali 7:3" Basi mbona wakitazama kibanzi kilichoko ndani ya jicho la nduguyo na boriti iliyoko ndani ya jicho lako mwenyewe huliangalii".
Yeremia 1:11" Tena Neno la Bwana likanijia kusema Yeremia waona nini, nikasema naona ufito wa mlonzi ( maana yake ni mateso)". Sasa mtesi mkubwa ni wewe mwenyewe! Yesu anasema liangalie hilo boriti jichoni kwako; yakupasa kufahamu kwamba unatakiwa kuyatatua yale yanayokuhusu kabla hujaanza kuyatatua ya mwingine. Tusiwe watu wa kuangalia huku na huku na kusema, " Yule anadhambi sana, yule anashida sana", hebu uwe mtu wa kuangalia ya kwako alafu uone unaweza kutoka mahali kwenda mahali. Hebu angalia yale unayoweza kuyatatua. Tafuta kwa bidii kujua yanayokuumiza kabla hujashughulikia yamuumizayo mwenzako maana yawezekana matatizo yako yanasababisha wengine wateseke au waumie.
MTUMISHI WA MUNGU MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA - EFATHA MINISTRY.

Comments