Muda umefika wa KUDHIHIRISHA NGUVU zake YEYE aliye juu. Hutatishiwa na Umaskini, Mapepo, Uchawi wala ajali haita kutisha, JITAMKIE kuwa “Mimi ni mbeba INJILI na Hakuna cha Kunitishia”. Hutatishiwa na maradhi wala magonjwa kwa kuwa Mwili wako ni HEKALU la Roho Mtakatifu.

Muda unakuja na sasa UMEFIKA; Udhihirisho wa ROHO MTAKATIFU uko ndani yako, magonjwa na mateso hayatakusumbua. Wewe ni MAALUMU kwa ajili ya UFALME wa Mungu.

Umekaa kwa muda mrefu ukiwa Unateseka na Vitisho vya kila aina na Umaskini umekusumbua, umekuwa usiyejua wapi Utakula, Utavaa nini au Utawapelekaje watoto wako shuleni; kipindi hicho Kimekwisha BWANA Amekukumbuka na WEWE. 
TEMBEA kifua mbele huku ukijua kuwa BWANA yupo Pamoja nawe.

© MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA (EFATHA MINISTRY).


Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."