SOMO: TOFAUTI KATI YA MWANA NA MTOTO
Yohana1:12" Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio Jina lake". Ni vizuri ukafahamu tofauti ya MWANA na MTOTO na mazingira unayokwenda nayo. Tukimpokea Yesu Kristo; tunaitwa watoto wa Mungu na tukiendelea na WOKOVU, tunaitwa WANA wa Mungu. Watoto ni wale wasioelewa Neno la Mungu kwa kina. Biblia inasema wananyonya maziwa, hawajajua kupambanua Neno bado.
Ukiwa mtoto, unarushwa huku na kule, maana huna maamuzi, lakini unajengwa utoke kwenye utoto mpaka unafikia ukamilifu kwenye nafasi aliyoko Kristo. Wakamilifu ndio wanaoitwa WANA, ambao wanatenda kile angefanya Bwana Yesu, kama angekuwepo. Hawaitaji aje, bali wao wapo na wanamwakilisha Yesu hapa duniani. Kwa hiyo mtaani kwako ni lazima uonyeshe Bwana Yesu yupo.
Waliookoka ni jeshi la Bwana, na wale wachanga ni makuruta ambao hawajafika hatua ya kuwa maafande.Wakishamaliza hiyo hatua ya ukuruta na kufuzu, wanakuwa maafande, napo wanapanda daraja mpaka wanakuwa majenerali wakuu.Taka kupanda daraja na inategemea unavyokabili mambo au changamoto. Mtu akisha kuwa MWANA haangaiki kutafuta maombi maana Mungu ameshamtoa chini na kumpeleka juu.
   : Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira (EFATHA MINISTRY).

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."