SOMO: ROHO WA BWANA JUU YETU.

Roho wa Bwana juu yetu, amebeba mambo Mawili makubwa, nayo ni KUMTAMBULISHA MUNGU KWA WATU na KUPAKA WATU MAFUTA; ambapo Mungu hutupaka Mafuta kupitia kwake. Yesu alisema Roho wa Bwana yu juu yake, ili kumtia Mafuta apate kuwahubiria maskini Injili au Habari njema. Apate kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao na vipofu kupata kuona tena. Awaache huru waliosetwa na kutangaza Mwaka wa Bwana uliokubaliwa.
Luka 4:18-19 "Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia Mafuta kuwahubiria maskini habari njema, amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao......".

Roho wa Bwana alikuwa juu yake akimmiminia mafuta, sio ndani yake; kwa sababu alitumwa na Mungu aliye BABA yetu, ambaye ndiye Mmiliki wa Mbingu na Nchi. Hiyo Mamlaka aliyonayo Mungu, amempa Bwana wetu Yesu Kristo ili apate kuwapa wale walio tayari kumtumikia Mungu, siku za uhai wao. 

Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."