SOMO: ROHO WA BWANA JUU YETU.

Roho wa BWANA juu yetu, ni moja ya Roho saba za Mungu zinazotenda kazi duniani, ambaye alihusika kuumba Mbingu na Nchi.
Mwanzo 2:4 "Hivyo ndivyo vizazi vya Mbingu na Nchi zilipoumbwa. Siku zile BWANA Mungu alipoziumba Mbingu na Nchi". Vile vile ni kati ya Roho mbili zinazotolewa na Mungu mwenyewe, nyingine ni Roho wa Kumcha BWANA. Roho wa BWANA juu yako ni ili kukuwezesha kufanya Utumishi kwa Mungu wako aliyekurahisishia Maisha kwa kukupa Roho wake.

Warumi 8:14 "Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu." Baada ya kufanyiwa hayo yote ndipo Mungu huruhusu Roho ya Kumcha BWANA, ili upate Kumcha YEYE, yaani upate kuwa na Ibada na Mungu wako.
Mithali 8:17 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona." 

Mathayo 5:8 "Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu." Kumpenda Mungu ndiyo moyo safi.

Inaendelea.....

Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira - Efatha Ministry.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."