SOMO: KUZINGATIA.
Luka 15:14-18" Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile, naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. ALIPOZINGATIA MOYONI MWAKE , akasema, Niwatumishi wangapi wa baba yangu wanaokula Chakula na kusaza....."
Mwana mpotevu alipozingatia moyoni mwake akafanya maamuzi yakurudi kwa baba yake. Kuna watu wanasema siwezi kuacha pombe, sigara, uzinzi au uasherati hii ni vita huwezi kuacha kirahisi lazima useme SITAKII. Kuna watu hawawezi kuishi maisha matakatifu kwa sababu ya vitu vya kupewa, wanapenda vitu vitamu, anasema nitaishije nikiacha dhambi?? Hebu amua kutoka hapo uone, MUNGU hatakuacha uaibike. Amua kufanya maamuzi ya hatari ili utoke kwenye hali inayokusumbua. Amua kurudi kwa BABA yako ambaye dunia na vyote viijazavyo ni mali yake, usiendelee kula na nguruwe wakati nyumbani kwa baba yako kuna utajiri wa kila aina.
   
   - Mtumishi wa Mungu Mama Eliakunda Mwingira -EFATHA MINISTRY.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."