SOMO: USIDHARAU UUMBAJI WA MUNGU.
Kila alichoumba MUNGU kinakubalika mbele zake na kina Kusudi maalum kwa ajili yake, tena ni Watumishi wake. Ndani ya hicho kiumbe ameweka hazina ya VIPAWA.
Kwa hiyo usimdharau mtu kwa kuwa hujajua bado kesho atakuwa nani? au ana nini kitakachokusaidia au kukuokoa wakati wa uhitaji wako?
Tamani wengine wafikie Kusudi la Mungu katika Maisha yao kwa kuwasogeza karibu na Bwana. Chochote ambacho Mungu amekiweka mkononi au mbele yako, pokea na kitunze kwa shukurani kwa kuwa Kazi ya Mungu haina makosa.
Katika Biblia Nabii Balam aliokolewa na punda ambaye alimwona Malaika aliyetaka kumuua; Lakini yeye (Balam) hakumuona. 
Mungu anaweza kutumia kitu chochote ili kutimiza Mapenzi yake, maana anajua kila kinachotokea.
Mhubiri 7:13, "Tafakari vema kazi yake; kwa sababu ni nani awezaye kukinyoosha kitu kile alichokipotosha yeye?"
   -: Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."