Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira:
Mungu anatafuta watu wanyenyekevu, walio tayari Kumwabudu ambao wanatetemeka wasikiapo habari zake. Kumcha BWANA ni kuchukia uovu na chochote kisichompendeza Mungu. Hali hii hukupa kuwa ushirika na Mungu, unaokufanya Kumpenda Mungu, Kumheshimu, Kumwabudu na Kumtumikia bila kulazimishwa. Unakuwa tayari kujitaabisha, kujituma na kujibidiisha kwa ajili ya BWANA, kwani ndiyo furaha yako. Unatimiza ahadi zako bila kuhimizwa, naye anatawala Maisha yako. Mtu wa Mungu anatakiwa awe na tabia hiyo, hahitaji abembelezwe ili amtumikie Mungu, awahi ibadani au amtolee Mungu. Unajua shida uliyonayo, kwa hiyo tenda kwa hiari ili ajibu haja ya moyo wako.
Ukimpenda Mungu na kumtumikia kwa uaminifu na kweli; na kuwa na adabu mbele zake, utakuwa salama, mbali na uchungu, mahangaiko na kuonewa.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."