MKESHA WA UDHIHIRISHO WA NGUVU ZA ROHO MTAKATIFU, EFATHA MINISTRY PRECIOUS CENTER KIBAHA,
Luka15:17 “Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.”
Mwana mpotevu alipata nafasi kwa Baba yake lakini akaichezea, ndiyo maana baada ya kuipoteza akajuta na kukumbuka nyumbani kwa baba yake, alijua kuwa nyumbani kwao kuna kila kitu ndiyo maana akaamua kurudi kwa Baba yake.
Vivyo hivyo ndivyo ilivyo Nyumbani mwa BABA yako wa Mbinguni, kuna chakula cha kutosha; rudi nyumbani kwa BABA yako ili uweze kupokea chakula kutoka kwake maana kwake kuna kila kitu unacho kitaka, ikiwemo Karama na Vipawa vya Roho Mtakatifu na chochote kile unacho kihitaji kinapatikana kwake.
© MCHUNGAJI BETSON KIKOTI.

Comments