USHUHUDA:
Ester Musa, natokea Kimara.
Kwa muda wa mwaka mmoja nilikuwa nahisi tumboni kuna kitu kinatembea na nilipokwenda Hospitali nikaambiwa kuwa mimi ni mjamzito japo nilikuwa naona siku zangu kama kawaida.
Nilikuwa naingia kwenye siku zangu kwa siku tano lakini baada ya hali hii nikawa napata hedhi kwa siku mbili na damu ikawa ni kidogo sana. Nilipokuja katika Kusanyiko hili linaloendelea Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira akasema kuwa "kuna mtu anahisi kama ana mtoto tumboni lakini huyo si mtoto bali ni pepo kuanzia saa hii uwe huru kwa Jina la Yesu".
Mtu huyo alikuwa ni mimi nikapokea uponyaji saa ile ile. Napenda kumshukuru Mungu kwa kuniponya katika Kusanyiko hili, nimeuona mkono wake hata kabla kusanyiko halijaisha..

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."