SOMO: BADILISHA TABIA ZAKO:
Wokovu ni kubadilika, inaumiza sana kuona mtu ameokoka na bado anaendelea na tabia za watu ambao hawajaokoka, hii inawafanya wale ambao hawajaokoka wakikuangalia wanasema kama kuokoka ndio hivyo basi.
Imeandikwa kumpenda Mungu ni kuuchukia uovu. Wewe ambaye umeokoka umefanyika kuwa balozi wa Yesu hapa Duniani, watu hawamuoni Yesu bali wanakuona wewe, hivyo hakikisha tabia zako zinafanana na Yesu.
Leo mwambie Yesu najichomeka kwako ili tabia zangu zifanane na Wewe, watu wakiniona waone wamekutana na Yesu.
Mtumishi wa Mungu Mama Eliakunda Mwingira.

Comments