MTUMISHI WA MUNGU MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA :
Kamwe usijinenee mabaya kwani itakuwa kama ulivyo jitamkia, unakuta mtu anakiri " siku hizi maisha ni magumu sana " unapo kiri hivyo kamwe maisha yako hayataweza kuwa Mazuri, kwa sababu umejitabiria maisha magumu mwenyewe.
Usijitabirie mambo mabaya, mara nyingi akina Dada mnaweza kuwa na marafiki zenu mnaanza kusema, wanaume ni wabaya sana, alafu unataka kuolewa, hapo usitegemee kupata mume mzuri.
Vijana wengine wanasema wanawake ni wasumbufu sana, ukisema hivyo usitarajie kupata mke mtulivu bali tarajia kupata kama yule uliyejitabiria mwenyewe.
Unapaswa kuwa makini sana na maneno ya kinywa chako, chochote utakacho kiri kitakuwa kama ulivyo kiri.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."