HALELUYA, HALELUYA, HALELUYA Kusanyiko TAKATIFU la Mwaka huu 2017 wa Kujibiwa MAOMBI Linakaribia. Kusanyiko litaanza tarehe 2/October - 8/ October, Kibaha Precious Centre Mji wa BWANA.
Kwa Wale ambao ni Wageni (Si Wana Efatha Ndani ya Tanzania na Nje ya Tanzania) na wengependa kuja KUPOKEA kile ambacho BABA YETU KIPENZI WA MBINGUNI Alichoandaa kupitia Wapakwa Mafuta wake wakiongozwa na Mtumishi wake Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, unapaswa KUJIANDIKISHA (REGISTER YOUR DETAILS) kupitia Website ya Huduma ambayo ni www.efathaministry.org kwa ajili ya Maandalizi ya Nafasi yako ya HOTEL (Malazi na Chakula) na kama pia utakuja na kuondoka (yaani hutalala) pia unapaswa KUJIANDIKISHA kwa ajili ya Utaratibu wa USAFIRI.
Mwisho wa Kujiandikisha ni tarehe 22/ September Mwezi huu.
Ukisha JIANDIKISHA utapokea E-mail yenye maelezo yote, pia unaweza kupata Maelezo yote katika Website yetu ya Huduma.
UBARIKIWE Mwana wa Mungu, YESU Anakupenda, YESU Anakujali.
"SHARE IT"...... na Mkaribishe na Mwenzio (Mke wako, Mume wako, Wazazi wako, Ndugu zako, Jirani zako, Wafanyakazi wenzio, Wanafunzi wenzako, Wafanyabiashara wenzako n.k.) na wale wooote ambao bado hawajampokea Bwana wetu YESU KRISTO kama BWANA na MWOKOZI wa Maisha yao, na Wooooote wenye Mapenzi Mema.
KARIBU, tunakusubiri Kukuona, KARIBU.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."