MAMA ELIAKUNDA MWINGIRA:
MUNGU wetu ni Mungu wa Mpangilio na Mwaminifu, Mungu ana Mpango na wewe, haijalishi unapitia magumu gani LEO unapaswa kujua Mungu AMEKUSIKIA kilio chako.
Yumkini umefika mahali umekuwa mbali na YEYE ni kwa sababu ulifanya Maovu ambayo yamekupeleka uwe kwenye mateso. Maisha ya uovu ndiyo yanayokupelekea uingie kwenye Maumivu.
Ishi Maisha ya KUMPENDEZA Mungu ili Umfurahishe YEYE ili Akutoe kwenye Maumivu na Mateso unayopitia.
Huu ni Mwezi wa Maombi, unatakiwa kutembea katika UTAKATIFU ili Umuone Mungu, zingatia wakati huu tuliopewa kwa KUJINYENYEKEZA mbele Zake ili Akuondolee hayo Mateso na Magumu unayopitia, ukitembea katika UTAKATIFU Mwezi huu Hautapita bure bali YEYE ATAKUONDOLEA Maumivu na Mateso unayoyapitia.
MUNGU wetu ni Mungu wa REHEMA, YEYE Anasamehe maana hata mchawi anayewanga Akitubu Mungu anasamehe. Mtu wa Mungu geuka, ACHA Dhambi na Kuishi Maisha ya KUZOELEA dhambi. ROHO MTAKATIFU ndiye Anayetupa KUTUBU na KUTENGENEZA lakini ukimtia kisirani Anaondoka na Anakuacha.
Wewe ULIYEOKOKA ACHA Dhambi, unayesema Bwana YESU Asifiwe lakini ni MDOMONI tuu wakati Moyo umeuelekeza mahali pengine kwenye uongo, usengenyaji, au kwa mke mdogo hiyo ni DHAMBI. Moyo una ugonjwa wa Kufisha, BADILISHA Tabia yako.
Ukimpata ROHO MTAKATIFU Atakupa dira wapi unatakiwa uende, Akiingilia Maisha yako ATAKUBADILISHA.
Kipindi hiki cha Maombi Atakubadilisha Usiangalie Mazingira, Usitegemee Akili zako wala Usimtegemee mtu maana imeandikwa kuwa "Yeyote amtegemeaye mwanadamu amelaaniwa", MUAMINI na UMTEGEMEE YEYE TU naye Atabadilisha Maisha yako nawe utakuwa BORA kati ya Walio BORA.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."