IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA NANE:
MTUMISHI: ADVESTA MLENGUS.
Yohana 15:16 “Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.
Bwana YESU alituombea kwa BABA ili tulindwe na Yule mwovu kwa sababu alikuwa anajua kuwa AMETUCHAGUA na KUTUWEKA ili tufanye KAZI YAKE. Si wewe uliyejichagua na kujiweka hapo ulipo na kwenye nafasi uliyonayo bali ni YEYE aliyekuchaguwa. Mungu hawezi kukupa kitu ambacho hukiwezi kukifanya, wewe uliye Kiongozi fahamu kuwa Alikuchagua kabla ya kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.
Tunapaswa kuwaheshimu Viongozi waliowekwa mbele yetu, Mchungaji, Askofu Kiongozi wa cell n.k, kwa maana wao hawakujichagua bali ni Bwana YESU. Ukijua kuwa kiongozi wako aliwekwa na nani katika nafasi aliyoko Utamuheshimu.
Mathayo 22:14 “Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.” Usikae katika nafasi ya kuitwa bali kaa katika nafasi ya kuteuliwa, ukikaa hapo Utamuheshimu aliye mbele yako yaani (Kiongozi wako). Unapaswa kumuheshimu na ukimuheshimu Yeye utakuwa ni sawa na Kumuheshimu yule aliyemuweka ambaye ni MUNGU.
Kiongozi usipoitunza nafasi yako na kukaa vizuri Mungu akikutoa hapo anamuweka mwingine, kubali kile ulichopewa ukitendee Kazi kwa UBORA, UHODARI na USHUJAA.
Mungu anawachukia watu Wavivu wale wanao tenda kazi kwa ULEGEVU.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."