IBADA YA KUFUNGA NA KUOMBA SIKU YA NANE:
MTUMISHI: ADVESTA MLENGUS

ZABURI 75:1 “Ee Mungu, twakushukuru. Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu; Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.”
Unapaswa KUMSHUKURU Mungu kwa kila kitu alichokupa katika Maisha yako, MSHUKURU kwa Pumzi aliyokupa maana pasipo YEYE huwezi Kuishi, YEYE ni chanzo cha UHAI na UZIMA wako. Mungu anafurahia MOYO wa SHUKRANI hivyo ili UMPENDEZE inakupasa uwe na Moyo wa SHUKRANI mbele zake.
Muombe Mungu akupe NGUVU yake ili uweze Kutenda yale aliyokupa katika UBORA, UHODARI na USHUJAA pasipo Woga wowote, maana bila NGUVU yake huwezi Kufanya kitu chochote. Hiyo NGUVU ikikushukia inakupa kufanya Mambo yako kwa URAHISI na WEPESI zaidi. Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika YEYE anitiaye Nguvu. ”

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."