USHUHUDA

Naitwa Khadija Makani, napenda kumshukuru MUNGU kwa MATENDO yake ya Ajabu aliyonitendea. Nina miaka sita nilikuwa natoa funza katika sehemu zangu za siri, nilihangaika sana kutafuta UPONYAJI lakini sikupona hadi ndugu zangu wakanisusa wakasema huyu mtu kufa hafi wala haponi wakaacha kunihudumia. Nikawa nimekaa ndani tu nateseka ila kuna Mama mmoja akanipeleka Hospitali lakini ugonjwa haukuonekana, ndipo nilipoletwa Efatha Nikaombewa na baada ya Maombi nilipoenda Hospitalini ndipo ugonjwa Ukaonekana. Nikagundulika nina uvimbe tumboni nikafanyiwa upasuaji Nikakatwa utumbo nikawekewa wa plastiki, ndipo nikagundulika na Kansa tena nikawa naendelea na Matibabu huku nakuja kwenye Maombi. Nilipoenda Kupima tena wakaniambia kuwa NIMEPONA na hata dozi ya dawa sijamaliza, NAMSHUKURU sana MUNGU kwa MATENDO YAKE aliyonitendea sitarudi nyuma bali NITAMTUMIKIA huyu MUNGU wa Mbinguni, Namrudishia SIFA na UTUKUFU, YEYE MUWEZA wa Yote.

JE? Wewe una tatizo gani??? Uwe na AMANI, YESU anaponya... KARIBU KWA YESU UPOKEE UPONYAJI WAKO.
Achana na maneno ya kukatisha tamaa YESU YUPO NA ANAPONYA HATA SASA.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."