PASTOR MICHAEL OLAWORE KUTOKA UK (KATIKA KUSANYIKO KUU 2016) Mungu anatangaza mwisho tangu mwanzo, katikati ya ukame, njaa na hali ngumu isiyofuraisha MUNGU atakubariki. Yesu alikupenda hata akafa msalabani kwa ajili yako, na ni mpango wake yeye kukutoa kwenye huo ukame unaopitia. Katika hali yoyote unayopitia MUNGU hataacha kukupenda kwasababu asili yake ni Upendo na hakuna kinachoweza kumbadilisha. Mpango wa Mungu kwako ni mkubwa sana hata katika hayo maumivu unayopitia atakubariki. Amesema amekuchora kwenye viganja vya mikono yake na anakujua vizuri kiasi kwamba hata idadi ya nywele zako anaijua, na kabla hujaingia katika tumbo la mama yako alikujua. Kama hujui kama MUNGU anakupenda na kukujali ujasiri wa kuomba utapotea.


Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."