PASTOR MICHAEL OLAWARE KUTOKA UK (KATIKA KUSANYIKO KUU 2016) SOMO : KUVUNJA KIZUIZI MBELE YAKO Ukivunja vizuizi itakurahisishia kufika mbali kwa sababu mbele ya kuvunja mipaka kuna Baraka zako ila usipo vunja utabaki hapo ulipo. Maisha ya kawaida ni tatizo hakuna mtu aliumba kuishi maisha ya kawaida bali kipo kizuizi kinacho kuzuilia kufika mahali ambapo Mungu amekukusudia. Vikwazo ni:- 1. Mazoea : Amua kutoka kwenye aina ya maisha uliyoyazoea 2. Maoni ya wanadamu: Acha kusikiliza kile watu wanasema juu yako, kwama huwezi hiki au kile 3. Wewe mwenyewe kuwa kikwazo: Kujiona huwezi, eti kwa kuwa hujasoma, au familia yenu haijaifanikiwa. UKITAKA KUFANIKIWA LAZIMA USHINDE HIVYO VIKWAZO


Comments