MCHUNGAJI DAVID URIO. SOMO:BARAKA ZINAPATIKANA HEMANI MWA BWANA. Yoshua 1:9 "Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako". Mungu anasema tusiogope maana tumepewa Efatha na jina la Yesu kwa sababu jina la Yesu linafungua, linaponya na kuokoa. Zaburi 24:1-5 "Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake. Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari, Na juu ya mito ya maji aliithibitisha. Ni nani atakayepanda katika mlima wa Bwana? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake? Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila. Atapokea baraka kwa Bwana, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake". Utapokea Baraka kutoka kwa Bwana Mungu wa wokovu wako kupitia jitihada za kukaa kwenye uvuli huu wa Efatha, sikiliza kwa makini maagizo yanayotoka kwa Mtume na Nabii Josephat E. Mwingira na uyatendee kazi maana ndipo zilipo Baraka zako.

Comments