SHUHUDA Naitwa Mboni Mwaminifu namshukuru Mungu kwa Kumkomboa na Kumponya mwanangu kutoka katika nguvu za kichawi. Shetani alimtumia kuharibu vitu vingi na kufanya mambo mengi ya kipepo, tulihangaika makanisa mengi bila kupata msaada, lakini siku moja tukaamua kumleta hapa Efatha ambapo aliombewa na siku ya tarehe 14/8/2016 tulienda Precious Center Kibaha ambapo kulikuwa na Ibada, Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira alitamka kuwa kila uchawi na ulozi mwisho leo, na tukashiriki meza ya Bwana baada ya Ibada ile alitapika sana na sasa amekuwa mzima kwa kuwa amefunguliwa kutoka katika nguvu hizo ambazo alipewa na Bibi yake. Hakika Mungu ni mkuu na anatenda mambo ya ajabu Sifa na Utukufu namrudishia yeye aliye mwenye uweza wote.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."