Mchungaji Margareth Ilomo: WAOMBEE WANAOKUUDHI ILI UWE MKAMILIFU: Mathayo 5:43-48" Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki......" MUNGU hapendi KISASI NA KINYONGO kwasababu kisasi na kinyongo kitakumaliza wewe mwenyewe, na utakufa mapema kwa Presha na kisukari. Maudhi hayatoki kwa mtu wa mbali bali yanatoka kwa watu wanaokuzunguka kama Mume, mke, shemeji, kazini kwako na kadhalika na huo ndio uwanja wa ibilisi wa kufanyia kazi zake. Wewe uliyeokoka unatakiwa kujilinda, kaa katika wokovu kwa malengo na adui hatakupata.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."