MCHUNGAJI DAVID MWAKISOLE: KUBALI NA KUTII ILI ULE MEMA YA NCHI Zaburi 126:5-6 ” Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha. Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.” • Usipo kubali kupanda wakati wa maumivu sahau kuvuna, • usipo kubali kutii wakati wa maumivu sahau kuvuna. • Biblia inaweka wazi kabisa kuwa ili mtu avune kwa furaha ni sharti akutane na maumi, kwasababu Baraka alizopewa na Mungu aliziuza kwa adui haziko mikononi mwake hivyo ili kuzipata kuna maumivu, vita na ibilisi na atakaye shinda ndio atakaye zichukua hizo Baraka. • Unapoamua kumfuata Mungu na ukakutana na jambo lolote ambalo linakukatisha tamaa usiliangalie bali angalia palipo na Baraka zako, Nakutangazia ushindi kwa jina la Yesu.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."