IBADANI JUMAPILI TAREHE 22/03/2015

Mchungaji Mary Abel wa Eneo la Utukufu aliyeongoza Ibada ya Neno katika Ibada ya Kwanza..
 Efatha Mass wakimuimbia Mungu wetu, hakika wameimba kwa uzuri wa aina yake Mungu azidi kuwapaka mafuta kwa ajili ya utumishi wao. Amen
 Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira naye yupo katika Ibada hii ya kwanza ni Baraka ya pekee kuwa na Baba yetu. Amen
 Pichani: Mchungaji Thadeo Msuya akihubiri kwenye Ibada ya pili, Efatha Mwenge Dar es salaam.
 Watumishi wa Mungu kwa utulivu wakifuatilia Ibada ya Neno iliyoongozwa na Mchungaji Msuya.
 USHUHUDA
Hery Jackson, namshukuru Mungu kwa kunipa kibali fanya kazi yake Precious Center Kibaha, baada ya kufanya kazi kwa uaminifu, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira alinikabidhi kwa mtu mmoja akamwambia nenda na huyu kijana ukamfundishe kazi mpaka kitu kitokee, kweli baada ya hapo niliendelea na huyo mtu niliepewa akawa ananifundisha kazi ya uhandisi wa majengo na barabara na kweli kimetokea kitu kama baba alivyosema. Sasa nafanya kazi katika makapuni mbalimbali kama Mhandisi namshukuru Mungu kwa maana kwa elimu niliyonayo nisingeweza kufanya kazi kama hii ila ni kwa neema tu. Pili namshukuru Mtume na Nabii na mchungaji wangu Aimana Dominick kwahiyo nimekuja kushuhudia haya Mungu aliyonifanyia ili kuujenga ufalme wake, Amen.

Comments