IBADA KUU TAREHE 25/01/2015 EFATHA MWENGE.

Mchungaji kiongozi Kanisa la Efatha Mwenge Dar es salaam akifundisha katika Ibada ya kwanza.
USHUHUDA
Naitwa Vicent Sungura.
Mimi napenda kumshukuru Mungu kwa yale aliyonitendea, Baba alisema tukagombee nafasi mbalimbali kwenye maeneo tunayoishi nikagombea ujumbe wa serikali ya mtaa, mtaa wa mabibo, katika kura za maoni nilishinda kwa kishindo mpaka kusimama kuwa mjumbe. Pia napenda kumshukuru Mungu kuwa nilikwenda nyasa kwetu kutangaza nia ya kugombea udiwani nilipofika songea mjini nikapigiwa simu kwamba kuna kazi ya ICT Kigoma, baadaye nilipigiwa simu nikaambiwa kuna kazi nyingine Mwanza. Wakati naingia Efatha nilimuamini mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira nikaamua kushika maneno anayotufundisha nikaazimia mambo matatu, nilisema nitakuwa mwimbaji nimuimbie Mungu, imekuwa. Pia nilisema kwa namna yeyote nitasoma Mungu ni mwema nilipata mfadhili Naibu waziri wa miundo mbinu nimesoma mpaka chuo kikuu, nikasema nitafanya kazi nitakayoichagua yenye maslahi. Namshukuru Mungu leo hii nachagua kazi, naenda Mwanza nikiona maslahi siyo mazuri naenda Kigoma. Ukiwa ndani ya Efatha jitahidi kushika Neno la madhabahuni Mungu atalithibitisha Neno lake, Amen.
 Watumishi wa Mungu wakifatilia neno kwa makini.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."