SOMO: KUSIKIA NA KUONA (Linaendelea tulipoishia) Zaburi 1:1a [Heri mtu Yule asiyekwenda katika shauri la …] ukianza kusikiliza umbea nina uhakika kile ambacho unacho kitaondolewa, unaweza kusikia Efatha hawakupendi na wewe ukaamini, utakuwa umepotea, sikiliza “EFATHA NI YESU sio watu”. 1Timoteo 4:1 [Roho zidanganyazo…] ukifika mahali umempokea YESU ukiruhusu muovu aingie na kulichukua Neno ni hatari sana. Miiba ni wale ambao wanasikia na wanaona lakini kutokana na shughuli nyingi za kidunia walizonazo na udanganyifu wa mali wanashindwa kuzaa kwa sababu hawana muda wa kutafakari uzuri wa MUNGU na kufanya mapenzi ya MUNGU. Makundi yote haya manne wote walimpokea YESU, wasingempokea asingesema “…muovu akaja na kuiba”. Yohana 15:6 [Mtu asipokaa ndani yangu…] Anasema mtu “asipokaa” ndani yangu; hasemi “hakunisikia”, kwani hujawahahi kuona mtu amekuja nyumbani kwako ukamkaribisha, akaingia lakini ukimkaribisha kiti anasema ana haraka hakai.: Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.

Comments

Popular posts from this blog

Mithali 8:17-21 "Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, na faida yangu hupita fedha iliyo teule. Natembea katika njia ya haki, katikati ya mapito ya hukumu. Niwarithishe mali wale wanipendao, tena nipate kuzijaza hazina zao." Proverbs 8: 17-21 "I love them that love me; and those that seek me early shall find me. Riches and honour are with me; yea, durable riches and righteousness. My fruit is better than gold, yea, than fine gold; and my revenue than choice silver. I lead in the way of righteousness, in the midst of the paths of judgment: That I may cause those that love me to inherit substance; and I will fill their treasures."